.

.
Tuesday, October 30, 2012

1:54 PM

Ghasia zilizuka baada ya kifo cha Kwega mjini Kisumu

Mwanasiasa wa Kenya Shem Kwega ameuawa huku mke wake akijeruhiwa mjini Kisumu Magharibi mwa Kenya.
Bwana Kwega alikuwa mshirika wa karibu wa waziri mkuu, Raila Odinga, anayegombea urais.
Polisi waliwarushia gesi ya kutoa machozi waandamanaji waliokuwa wanaelezea kero lao kuhusu mauaji hayo wakidai kuwa yalikuwa mauaji ya kupangwa.
Hali ya taharuki inatanda nchini Kenya kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika mwezi Machi.
Zaidi ya watu 1,000 waliuawa kwenye ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007 zilizofuatia uchaguzi uliozua utata mkubwa kuwahi kushuhudiwa nchini Kenya tangu uhuru.
Wiki jana kiongozi wa mashtaka katika mahakama ya kimataifa ya ICC, Fatou Bansouda alielezea wasiwasi kuhusu tatizo la vurugu nchini humo.
Mahakama ya ICC itawafungulia mashtaka washukiwa wanne wa ghasia hizo za baada ya uchaguzi akiwemo naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta ambaye pia anawania urais kwa kuhusika na ghasia hizo.
Bwana Kwaga na mkewe walipigwa risasi na washukiwa waliokuwa wanaendesha pikipiki.
Aidha marehemu Kwega alikuwa mfanyabiashara maarufu ambaye alikuwa anagombea kiti cha ubunge kwa chama cha waziri mkuu.
Ingawa polisi wangali wanashuku kuwa huenda kilikuwa kitendo cha wizi, lakini wafuasi wake wanaamini kuwa yalikuwa mauaji ya kupangwa.

0 comments:

Post a Comment