.

.
Monday, October 29, 2012

6:16 AM

KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA, LIBERATUS SABAS ALIPOKUWA AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI (HAWAPO PICHANI) MAPEMA LEO OFISINI KWAKE JUU YA MSAKO WA LEMA

Jeshi la polisi mkoani Arusha linamsaka aliyekuwa mmbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kwa tuhuma za kushambulia mwili pamoja na upotevu wa simu pamoja na fedha.

Akiongea na waandishi wa habari jijini hapa kamanda polisi Lebaratus Sabas alisema kuwa  jeshi la polisi linamsaka lema na wenzake ambao idadi yake hawajatajwa kwa tuhuma za kushambulia mwili wa watu wawili tukio lililofanyika october 28 mwaka huu katika kata ya daraja mbili.

Alisema kuwa jeshi la polisi lilipokea taarifa za malalamiko  kutoka kwa watu wawili waliojulikana kwa jina la Ibrahimu Juma pamoja na Maritin Daniel wote wakazi wa daraja mbili kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo la arusha mjini Godbless Lema akiwa na wanzake walimvamia na kuwashambulia kwa ngumi pamoja na kuwanyanganya simu aina ya samsang yenye samani ya shilingi laki tatu pamoja na fedha taslim kiasi cha shilingi laki mbili kisha kuondoka na kuwaacha.

Alisema kuwa watu hao waliamua kutoa taarifa polisi na jeshi la polisi linamsaka lema kwa ajili ya kujibu tuhuma hizi .
Gazeti hili lilimtafuta lema kujibu tuhuma hizi akupatikana kwani simu yake ya kiganjani ilikuwa imezimwa.

wakati huo huo jeshi la polisi linaashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na vitambulisho feki wakati wa uchaguzi wa udiwani wa kata ya daraja mbili uliofanyika jana jijini hapa.

Akizungumzia tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha aliwataja watu hao kuwa ni pamoja na Amosi Rajabu ambaye alikutwa akiwa na kitambulisho bandia chenye namba 45036846 huku mungine akijulikana kwa jina la Lukas Thomas manya ambaye naye alikamatwa na kitambulisho bandia ambapo alisema namba yake ilikuwa imefutika .

Alisema kuwa watuhumiwa wote hawa wapo chini ya ulinzi wanashikiliwa na jeshi la polisi  kwa ajili ya upelelezi na pindi utakapo kamilika watafikishwa mahakamani .

0 comments:

Post a Comment