.

.
Wednesday, October 31, 2012

1:02 PM
Mkurugenzi wa shirika la chakula duniani (FAO) Jose Graziano da Silva wakati wa kikao kwenye makao makuu ya FAO Italy. 
 
Idara ya Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO linazitaka serikali kuunga mkono masoko ya kilimo  ili kukabiliana na ongezeko la bei ya chakula duniani.

Akizungumza  Jumanne mjini Roma katika maadhimisho ya  siku ya chakula duniani  mkurugenzi mkuu wa idara hiyo  Jose Graziano  da Silva amesema,   ni muhimu kuimarisha usimamizi wa chakula kwa sababu hakuna nchi pekee inayoweza kujitosheleza  katika dunia ya leo ya utandawazi.

Aliwaambia mawaziri kutoka nchi 20 waliohudhuria  kikao hicho kuwa ipo haja ya kuibuka  kwa mtizamo mpya wa dunia unaoratibiwa kimataifa kwa kupashana habari na kuwa na uwazi katika masoko, ili kukimu mahitaji ya dunia ya chakula.

Aidha shirika hilo limesema  mashirika ya kilimo ya kijamii ni muhimu kwa sababu yana malengo ya kuimarisha jamii zake kwa kutumia raslimali ilizonazo kwa maslahi ya kijamii. FAO linakisia kuwa watu milioni 870 hukabiliwa na  njaa duniani, idadi inayosema ni ya juu mno, ingawa imeshuka kutoka watu bilioni moja mapema miaka ya tisini.

0 comments:

Post a Comment