.

.
Monday, October 29, 2012

2:53 AM
Kimbunga Sandy

Rais wa Marekani Barack Obama, amewatahadharisha wamarekani kuchukulia kwa uzito kimbunga Sandy huku maafisa wakianza kufunga eneo la Mashariki mwa pwani ya nchi hiyo wakisubiri kimbunga hicho kupiga.
Majimbo kadhaa yametangaza hali ya hatari huku mamilioni ya watu wakiathiriwa na dhoruba kali wakati shule na barabara zikifungwa.
Aidha Wataalamu wanahofia kimbunga hicho huenda kikawa kikali mno wakati kitakapopiga sehemu za nchi hiyo.
Baadhi ya mikutano ya kisiasa ya hadhara imesitishwa huku Rais Obama akionya watu kuchukua hatua za kujikinga na athari za zaidi za kimbunga hicho.
Usafiri wa kimataifa kutoka nchini humo umeathirika sana. Mashirika ya ndege ya Ufaransa, Uingereza na Virgin Atlantic yamesitisha safari zao katika baadhi ya sehemu za nchi hiyo ikiwemo miji ya , New York, Baltimore, Newark, Washington, Boston na Philadelphia kuanzia leo.
Kwa mujibu wa idara ya utabiri wa vimbunga, saa nane asubuhi ya leo, kimbunga hicho, kilianza kuelekea Kaskazini kikienda kwa kasi ya kilomita 760, Kusini Mashariki mwa mji wa New York.
Hali ya tahadhari imetangazwa katika miji ya Maryland, New York, Pennsylvania, Virginia, Washington DC na North Carolina.
Kimbunga hiki kinatoa fursa kwa Rais Obama kuonyesha uongozi wake mbali na siasa na ikiwa atakosa kuonyesha uongozi unaostahili huenda wakosoaji wake wakatumia fursa hiyo kumponda na kumlaumu kwa kosa lolote.

0 comments:

Post a Comment