.

.
Wednesday, October 31, 2012

5:39 AM
mwanafunzi wa shule ya Kinyaki aliyekamtwa kwa amri ya mkuu wa mkoa,  baada ya kuandanama kushinikza mwalimu mkuu kuondolewa shuleni kwao
MKUU wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo amewasweka rumande wanafunzi watatu wa Shule ya Sekondari Kimnyaki kwa kutoridhishwa na maelezo ya sababu za  maandamano yao na wanafunzi wenzake hadi Ofisini kwake.
Wanafunzi hao waliokamatwa wakati wakijieleza kusudio la maandamano yao ni pamoja na Ezekiel Memiri, Losijaki Lunde, na Meshack Lomnyaki ambapo walisema kuwa wamekuwa wakinyanyaswa na walimu wao shuleni ikiwemo kuwafanyisha kazi za nyumbani kama ma-house girl.

Maandamano ya wanafunzi hao yalikuwa na lengo la kushinikiza Mkuu wao wa shule ya kinyaki mwalimu Mariam Chamle kuondolewa kwa kuwa chanzo cha matatizo shuleni hapo ikiwemo kushusha kiwango cha taaaluma shuleni hapo.

Mmoja wa wanafunzi hao, Meshak Lonyaki ambaye ni kaka mkuu wa shule hiyo alisema kuwa walimu wao wamekuwa chanzo cha wao kufeli kwa kutokuwafundisha darasani badala yake wanadai hela ya kuwafundisha masomo ya ziada(tution) na kuwatoza shilingi 10,000.

Mbali na hilo pia wanafunzi hao walisema  kuwa katika mtihani wao wa mock ya form two baadhi ya wanafuzi walirudishwa majumbani kwa kudaiwa michango midogomidogo na kutofanya mitihani huku baadhi yao wakirudishwa ingawa walilipa lakini muhasibu hakuwaandikia hivyo kutakiwa kuwasilisha risiti huku wanafunzi wenzao wakiendelea na mitihani na wengine waliopoteza risiti hawakufanya mitihani. 

mkuu wa mkoa wa Arusha, Magessa S. Mulongo(kushoto) akiwa n La Kamanda wa operesheni maalum wa jeshi la polisi, peter Mvula(katikati) pamoja na kamanda wapolisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas (kulia) wakiwasikiliza wanafunzi wakijieleza. (hawapo pichani)
Katika maelezo yao, Mkuu wa Mkoa alisema kwamba ni makosa makubwa kwa wanafunzi kukaidi ama kushindwa kufuata maagizo ya shule hasa yaliyoandikwa katika fomu zao za kujiunga na shule kwa kufuata masharti ya kulipa ada ambapo aliamuru wakamatwe.

“Askari kamata hawa jamaa weka ndani hawana heshima hata kidogo,haiwezekani wakaufanya mkoa wa  Arusha kama kiwanja cha michezo kwamba kila anayehitaji kucheza anaruhusiwa kufika, haya mambo hayawezekani hata kidogo, hivyo hawa watakiona cha mtema kuni na wakome kufika hapa… lazima utaratibu ufuatwe ili kila mmoja apewe haki ya kusikilizwa”alisema Mkuu wa Mkoa na kuongeza:

“Tena nataka kuchukuwa nafasi hii kupiga marufuku maandamano yote ya wanafunzi katika Jijini la Arusha, siwezi kukubaliana na suala hili hata kidogo, kuna viongozi wa serikali wapo shuleni,nyinyi mko huku,Mkuu wa Wilaya ya Arumeru yuko huko tayari kwa ajili ya kuwasiliza mmekimbilia kwa Mkuu wa Mkoa tena bila vibali vya maandamano”

Aliishia hapo mkuu huyo bila kutatua kero za wanafunzi hao zaidi ya kuwakamata waliojieleza, na kuwataka wanafunzi hao warudi shule haraka na wakichelewa atachukua maamuziya kufunga shule hiyo.

 Awali kabla ya wanafunzi hao kufika Ofisi ya mkuu wa mkoa walikutana na vikwazo vya Askari wa Jeshi la Polisi kwa kupigwa mabomu ya machozi mfululizo na kusababisha baadhi yao kujeruhiwa ambapo hata hivyo awali kamanda wa operesheni maalum wa jeshi la polisi, Peter Mvula alikana wanafunzi hao kupigwa mabomu hadi mmoja wao alipotoa moja ya bomu ambalo halikulipuka walilorushiwa ndipo walipokubali.
mmoja wa wanafunzi akionyesha moja ya bomu waliloliokota lililorushwa na polisi lakini halikulipuka, ikiwa kama ushahidi kuwa walipigwa mabomu ya machozi
Maandamano hayo  yaliyoanza juzi yana lengo la kumshinikiza Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya Kinyak aondolewe kwa kile walichodai kwamba anachangia kudidimiza maendeleo yao kitaaluma na kwamba anafurahia matokeo mabaya ya wanafunzi hao.
Baada ya Jeshi la Polisi kufanikiwa kuzuia maandamano hayo siku ya kwanza ya octoba 30 siku inayofuata wanafunzi hao walibuni njia nyingine ya kuandamana na kufanikiwa kufika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Arusha pamoja na kupigwa mabomu ya machozi na kusababisha wengine waliojeruhiwa kurudia njiani.
“Jana Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Nyerembe Munassa alifikia shuleni kwetu akatuambia kwamba angekuja kesho (yaani leo) kutusikiliza, tukamsubiri hadi saa nne bila mafanikio ndipo tulipobuni njia nyingine ya kuandamana, tukaamua kuondoka shule mmoja mmoja mpaka katikati ya mji, ndipo tulipokutana na askari hao ambapo walianza kuturushia mabomu ya machozi sisi tukawa tunanawa huku tukiendelea kuja ”alisema Ezekiel Memiri





0 comments:

Post a Comment