.

.
Wednesday, October 24, 2012

9:29 PM
BAADHI ya wakazi wa Kijiji cha Igombe, Kata ya Bugogwa katika Manispaa ya Ilemela, jijini Mwanza, wanajisaidia kandokando mwa Ziwa Victoria na kusababisha uchafuzi wa mazingira.

Hali hiyo imebainika hivi karibuni wakati wa ziara ya waandishi wa habari za mazingira walipotembelea eneo la mwalo wa Igombe na kujionea vinyesi vya binadamu vilivyotapakaa huku shughuli za kilimo zikiendelea.
Akizungumzia hali hiyo, Katibu wa Ulinzi wa Rasilimali za Ziwa Victoria (BMU), Samson Pamba, alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema tayari wameweka utaratibu wa kuwaadhibu wachafuzi na waharibifu wa mazingira kwa kuwatoza faini ya sh 45,000 kwa atakayekamatwa.
Alisema tatizo hilo bado ni kubwa kutokana na baadhi ya watu kuvunja sheria kwa makusudi, hali ambayo imekuwa ikisababisha wananchi wengi wa eneo hilo kuugua magonjwa ya kuhara, kutapika, kutokana na mazingira kuwa machafu.
“Wananchi wa eneo hili wamekuwa wakitumia maji ya Ziwa Victoria kuoga, kufulia, kuoshea vyombo na wakati mwingine baadhi yao hutumia maji hayo kwa ajili ya kunywa licha ya kwamba kuna visima ya maji ya kunywa,” alisema.
Wanahabari walishuhudia pia shughuli za uchimbaji mchanga kandokando mwa ziwa hilo zikiendelea licha ya mamlaka husika kusema kuwa zilishapiga marufuku shughuli hizo.

0 comments:

Post a Comment